Kuelekea Siku ya Wanawake Duniani
04 Mar, 2025

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Machi 8, 2025, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeendelea kutoa elimu ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora mkoani Arusha katika Viwanja vya TBA vilivyopo Mtaa wa Kaloleni, Kata ya Mianzini.
Wananchi mbali mbali wamejitokeza katika Banda la THBUB kupata huduma ya ushauri wa kisheria, elimu kuhusu haki za binadamu na misingi ya utawala bora katika viwanja hivyo.