ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

WANAWAKE THBUB WA WASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

09 Mar, 2025
WANAWAKE THBUB WA WASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

 

Wanawake wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) wameungana na wanawake  Duniani kote katika kuadhimisha  Siku ya Wanawake Duniani, ambayo kitaifa  yamefanyika katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid  Mkoani Arusha machi 8, 2025.

Maadhimisho hayo yameongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt.  Samia Suluhu Hassan ambaye alikuwa mgeni Rasmi wa Maadhimisho hayo.

Katika maadhimisho hayo THBUB imehimiza Jamii kuona umuhimu wa kushirikisha Wanawake katika mipango ya maendeleo na  kuhakikisha wanapata fursa na haki sawa na Wanaume. 

Wanawake THBUB walishiriki katika maadhimisho hayo, yaliyoongozwa na Kauli mbiu isemayo:
"Wanawake na Wasichana 2025: Tumeimarisha Haki, usawa na Uwezeshaji