ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

WATENDAJI WA KATA WATAKIWA KUZINGATIA HAKI NA USAWA KATIKA KUWAHUDUMIA WANANCHI

21 Mar, 2025
WATENDAJI WA KATA WATAKIWA KUZINGATIA HAKI NA USAWA KATIKA KUWAHUDUMIA WANANCHI

 

Mchunguzi Mkuu Msaidizi kutoka Tume ya Haki za Binadamu, Bw. Halfan Botea amewataka Watendaji wa Kata za Halmashauri ya Mji wa Babati kuzingatia haki, usawa, uadilifu, utawala wa kisheria, uwazi, ushirikishaji wa Wananchi wanapotimiza majukumu yao ili kujiepusha na ukiukwaji wa haki za binadamu  na misingi ya utawala bora.

Hayo ameyasema wakati akiwasilisha mada ya haki za binadamu na utawala bora wakati wa mafunzo kwa watendaji hao yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji Babati Machi 19, 2025.

Aidha amebainisha faida mbali mbali za kusimamia haki za Binadamu na Utawala Bora kuwa ni chanzo cha uwepo wa amani katika jamii na kuleta uzalishaji bora kwa Maendeleo ya jamii.

Kwa upande  Watendaji Kata wakielezea umuhimu wa mafunzo hayo,  wameeleza kuwa mafunzo ya haki za binadamu na utawala bora waliyoyapata yamekuwa na manufaa makubwa kwao, huku wakiahidi kuyatumia katika utekelezaji wa majukumu yao.


Aidha, Bw. Botea amebainisha faida mbali mbali za kusimamia haki za Binadamu na Utawala Bora kuwa ni  pamoja na  uwepo wa amani katika jamii na kuleta uzalishaji bora kwa Maendeleo ya jamii.